Changamoto wachimbaji wadogo wa dhahabu zishughulikiwe kuimarisha ...
Yapo mambo kadhaa yanayopaswa kuangaliwa kwa umakini ili kupunguza athari za kimaadili, kiuchumi na kijamii kwenye maeneo yenye wachimbaji wadogo kama ilivyoshuhudiwa wilayani Chunya. Halmashauri hii iliyopo mkoani Mbeya ni miongoni mwa wilaya zenye hazina ya madini ya dhahabu ambayo takwimu za mwaka 2016/2017 zinaonyesha kilo 546.59 zilizalishwa.